Sherehe ya kitaifa iliyofanyika Cambodia Huko Phnom Penh, Cambodia, yapata watu 50, ikijumuisha watu wenye mamlaka na viongozi na waheshimiwa, waliambatana na jumuiya ya Kibahaí katika tukio katika Ofisi ya Kitaifa kusherehekea miaka mia mbili ya kuzaliwa kwa Bab. Programu ilijumuisha usomaji wa barua kutoka Nyumba ya Haki ya Ulimwengu na kuangalia filamu ya Kuchomoza kwa Mwanga, vyote vilitoka maalum kwa sherehe za miaka mia mbili. Kundi la vijana pia lilionesha dansi ya kitamaduni na wimbo wa Khmer, lugha ya kitaifa, juu ya maisha ya Bab.