Sampuli ndogo kutoka miongoni mwa maonesho ya kisanaa yasiyohesabika yalioandaliwa na watu binafsi na jumuiya mbalimbali ulimwenguni kwa ajili ya tukio la miaka mia mbili tangu Kuzaliwa kwa Bahá’u’lláh.
Tamasha la maonesho ya sanaa na utamaduni lilifanyika Malaysia kufungua sherehe kati ya jamii ya wa-Bahá’í kwa ajili ya miaka mia mbili ya kuzaliwa kwa Bahá’u’lláh, likiwakilisha utofauti wa kazi za kisanii kutoka sehemu mbali mbali za nchi na maeneo ya jirani.